January 31, 2014


Hali ya ushindani wa kufunga mabao kwa mastraika wa Ligi Kuu Bara inazidi kupamba moto baada ya Kipre Tchetche wa Azam kufikisha mabao tisa ikiwa ni tofauti ya bao moja na kinara Amissi Tambwe wa Simba mwenye 10.


Tambwe amesema kuwa hajawahi kumuona Tchetche hata siku moja lakini kutokana na taarifa anazozisikia, anaamini kuwa ni straika mzuri ila akaahidi kupambana naye.

Alisema kuwa hali kama hiyo hutokea kwenye ligi yoyote yenye ushindani lakini ameupokea ushindani huo kwa mikono miwili na anaamini atafunga mabao mengi zaidi kwenye mechi zijazo.

“Ni hali nzuri ya ushindani na inaonyesha kuwa ni straika mzuri kutokana na spidi yake lakini na mimi pia nitafunga kama kawaida kila ninapopata nafasi ili niongeze idadi kubwa na mwisho wa msimu niweze kutwaa ufungaji bora,” alisema Tambwe.


Kwa matokeo hayo, Tchetche sasa amekwea mpaka nafasi ya pili akifungana na Elias Maguri wa Ruvu Shooting wakifuatiwa na Juma Luizio wa Mtibwa na Hamis Kiiza wa Yanga wenye mabao nane kila mmoja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic