January 31, 2014

 
MESSI (KATIKATI) AKIITUMIKIA SIMBA KATIKA MECHI DHIDI YA RHINO, JUMAPILI ILIYOPITA
Na Mwandishi Wetu
MAMBO yamekucha kwa kiungo nyota wa Simba, Ramadhani Singano ‘Messi’ baada ya klabu tajiri ya TP Mazembe ya Lubumbashi, DR Congo kuonyesha wazi kuwa inamtaka.


TP Mazembe tayari imetuma mtu ambaye amekuja nchini kwa ajili ya kumshuhudia Messi akiichezea Simba na ameeleza nia ya klabu hiyo.

Shushu huyo wa usajili wa TP Mazembe alikuwa uwanjani wakati Simba ikicheza na Rhino ya Tabora kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, Jumapili na kushinda kwa bao 1-0 lililofungwa na Messi.

Habari za uhakika zimeeleza mara baada ya mtu huyo kumshuhudia Messi akifunga bao na pia kukosa penalti amewaeleza viongozi wa Simba kutokana na nia ya klabu hiyo maarufu barani Afrika.

“Jambo hili bado ni siri kubwa, lakini TP Mazembe walimtuma mtu wao, huyo ndiye alitumwa mara ya kwanza kuifanyia umafia Simba kabla ya TP Mazembe kuja hapa kucheza.

“Alipokuja akamuona (Mbwana) Samatta na kuwaambia kuna mchezaji hatari, ndiyo maana uongozi wote wa juu wa TP Mazembe ukaja kuja kushuhudia mechi hiyo na kweli Samatta akafanya vizuri.

“Kutokana na hali hiyo huyo jamaa anaaminiwa sana, akirudi na kusema Messi yuko safi, basi jamaa watakuja kufanya rasmi mazungumzo na Simba,” kilieleza chanzo cha uhakika.

TP Mazembe sasa inamlipa Samatta kitita cha dola 10,000 (Sh milioni 16.5), kwa mwezi. Kama itafanikiwa kumpata Messi, basi huenda akachota kuanzia dola 3,000 hadi 5,000, kwa mwezi.


Messi amekuwa gumzo kuanzia mwanzo wa msimu huu kutokana na kiwango chake kupanda kwa kasi kubwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic