January 9, 2014

MSAFARA WA YANGA KWENYE UWANJA WA NDEGE WA KITAMAIFA WA JULIUS NYERERE, LEO ALFAJIRI
Mabingwa wa soka Tanzania, Yanga leo wameondoka jijini Dar es Salaam saa 10:35 alfajiri kwenda Antalya nchini Uturuki.


Yanga itaweka kambi Antalya kwa kipindi cha zaidi ya siku kumi na inatarajia kuwasilia Istambuli leo asubuhu na mchana itaunganisha ndege kwenda Antalya.
Yanga imeondoka na kikosi cha jumla ya wachezaji 27, jumla ni watu 33 ukijumlisha benchi la ufundi na kiongozi wa msafara Bwana Rupia.
Kocha Msaidizi, Charles Boniface Mkwasa ndiye aliongoza msafara kwa upande wa benchi la ufundi akisaidiana na kocha wa makipa, Juma Pondamali.

Hii ni mara ya pili kwa Yanga kuweka kambi katika mji huo lengo likiwa ni kujiimarisha kwa ajili ya mzunguko wa lalasalama wa Ligi Kuu bara.

Hivi karibuni, Yanga ilimtimua kocha wake Ernie Brandts na sasa iko kwenye mchakato wa kusaka kocha mpya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic