January 8, 2014





Wekundu wa Msimbazi Simba wametinga nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuichapa Chuoni ya Zanzibar kwa mabao 2-0.


Mrundi Amissi Tambwe na kinda Ramadhani Singano ‘Messi’ ndiyo waliofanya ‘mauaji’ hayo usiku huu kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar.

Simba chini ya Kocha Zravko Logarusic na msaidizi wake Selemani Matola ilionyesha soka la kuvutia na kuwapa wakati mgumu Chuoni.
Pamoja na kuonyesha juhudi lakini wakati fulani, Chuoni walilazimika kuutafuta kwa tochi ili kupambana na makali ya Simba ambao walionekana wako sawa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic