February 21, 2014



Kweli Al Ahly ni janja ya nyani, kwani pamoja na kupoteza mechi kadhaa za Ligi Kuu Bara, imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Super Cup.

Al Ahly imetwaa ubingwa huo kwa kuichapa CS Sfaxien ya Tunisia kwa mabao 3-2 kwenye Uwanja wa jijini Cairo huku Kocha Msaidizi wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa akishuhudia live.

Mkwasa alikuwa uwanjani hapo kukamilisha idadi ya mashabiki 30,000 waliokubaliwa na serikali ya Misri kuingia uwanjani hapo.

Kocha huyo na mchezaji wa zamani wa Yanga, aliongozana na Watanzania waliokuwa tayari kuisaidia Yanga kwa ajili ya utaifa na baadhi ya maofisa wa ubalozi.
Ben Youssef aliifungia Sfaxien katika dakika ya 12 na kuamsha dalili za ushindi kwa wageni  lakini mshambuliaji wa zamani wa Hull City, Mohamed 'Gedo' Nagy akaisawazishia
Amr Gamal akapiga bao la pili kwa Sfaxien katika dakika ya 54 baada ya mkongwe wa Ahly Wael Gomaa kucheza faulo.
Mzaliwa wa Cameroon, Moussa Yedan alipiga krosi safi kwa Gamal aluyepiga kichwa na kuisawazishia Ahly.
Baada ya bao hilo ilionekana kama Sfaxien hawana ujanja na kutoa nafasi kwa Al Ahly kwenda mwendo wa nyuki na kufanikiwa kupata bao la ushindi.
Mara ya mwisho Ahly ilikutana na Sfaxien, miaka mitano iliyopita katika kombe hilohilo la Super Cup, wazee wa Cairo wakashinda.

Kocha Mkuu wa Ahly, Mohamed Youssef alisema sasa wanarudisha nguvu kwenye ligi kwa kuwa wamepoteza mechi tatu katika mechi tisa walizocheza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic