February 24, 2014


Mabingwa wa Afrika, Al Ahly, wameishusha AC Milan ya Italia katika cheo cha kuwa timu yenye makombe mengi zaidi ya kimataifa.


Al Ahly ambao ni mabingwa wa Afrika, wanakutana na Yanga Jumamosi hii jijini katika mechi ya Ligi ya Mabingwa inayosubiriwa kwa hamu jijini Dar.

Ushindi wa Al Ahly dhidi ya CS Sfaxien ya Tunisia katika fainali ya Super Cup, umeifanya kufikisha makombe 19 na kuivuka AC Milan na Boca Junior ambazo zina 18.


Uongozi wa Al Ahly, tayari umetuma barua kuitaka AC Milan kuondoa maneno yaliyo kwenye nembo yake yaliyoandikwa kwa lugha ya Kiitaliano “il club piu titolato al mondo”, ikiwa na maana, timu yenye vikombe vingi vya kimataifa kuliko zote duniani.

Vikombe hivyo vya Al Ahly; vinane ni vya Ligi ya Mabingwa, vinne ni Kombe la Washindi, sita vya Super Cup na kimoja cha Afro-Asian cup.

Al Ahly ina maanisha sasa ndiyo yenye vikombe vingi zaidi vya kimataifa, sifa ambayo haijawahi kushindwa na timu yoyote ya bara la Afrika.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic