Kocha Mkuu
wa Ruvu Shooting, Tom Olaba, juzi alifanya kituko cha mwaka baada ya kuliacha
benchi na kwenda kujisaidia.
Kocha huyo
alifanya jambo hilo wakati timu yake ikiwa nyuma kwa mabao 6-0 wakati ilipokuwa
ikivaana na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, mchezo ambao
ulimalizika kwa Yanga kushinda 7-0.
Olaba
ambaye muda mwingi wa mchezo huo alikuwa amesimama, aliondoka taratibu kwenye
benchi la timu yake akaelekea vyumbani ikiwa ni dakika ya 75 ya mchezo huku
mashabiki wakimzomea.
Kocha huyu
raia wa Kenya akiwa vyumbani timu yake ilifungwa bao la saba, ambalo liliwekwa
kimiani na Simon Msuva, huku kukiwa hakuna mtu hata mmoja aliyesimama kwenye
benchi.
Zikiwa
zimebaki dakika tano kocha huyo alirejea kwa madaha na kukuta timu yake
imelambwa bao la saba.
“Mimi
nilikwenda ‘toilet’, kwani nikiwa kocha sitakiwi kujisaidia?” alihoji kocha
huyo mwenye mbwembwe na kuongeza:
“Niliwahi
kumuona hata rais akitoka na kwenda kujisaidia, kwa nini kwangu ionekane ajabu?”
0 COMMENTS:
Post a Comment