February 19, 2014


Aliyewahi kuwa kipa wa Simba na Ashanti United, Amani Simba, anatarajiwa kuondoka nchini leo Jumatano kuelekea Nampula nchini Msumbiji kwa ajili ya majaribio ya wiki moja.


Awali, Amani aliwahi kuliambia gazeti hili kuwa amestaafu soka lakini sasa amesema kuwa ameamua kurejea tena kwa kuwa ameona mwili wake bado una nguvu.

 Amani amesema  anakwenda huko kwenye majaribio hayo akiamini kuwa atafuzu kutokana na kwamba anaamini yeye bado ana kiwango na atafanya vyema.
Alisisitiza anakwenda huko akiwa na matumaini makubwa kuwa atafanikiwa.
“Siku ya Jumatano (leo), ninaondoka hapa nchini kuelekea Nampula nchini Msumbiji kwa ajili ya majaribio, bado wakala wangu hajanieleza ni timu gani lakini amesema inashiriki ligi kuu ya huko.

 “Ninaamini nitafuzu kwa sababu bado nina uwezo wa kufanya vizuri kutokana na kiwango changu na nimeamua kurejea upya katika soka na ninakwenda kuanzia nje halafu nitarudi tena hapa nyumbani,” alisema Simba.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic