February 19, 2014

KIM AKIWA NA TASSO MUKEBEZI

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen, amesifia kiwango cha timu changa kwenye ligi kuu, Mbeya City na kusema kuwa ndiyo timu iliyopo kwenye kiwango cha juu zaidi kwa sasa.


Kim amesema katika mechi alizofuatilia, Mbeya City ndiyo imekuwa kwenye kiwango zaidi huku timu nyingine zikitetereka katikati mwa msimu.

Kim alisema timu hiyo ni mfano wa kuigwa kwa timu zenye ndoto ya kupata mafanikio na kuuza wachezaji kama zilivyo Simba na Yanga.

“Mbeya ni mfano wa kuigwa, kwa maoni yangu ndiyo timu bora msimu huu. Wanacheza soka zuri na la kuvutia wala hawajatetereka licha ya kuwa ni timu changa.
“Ni mfano mzuri wa kuigwa kwa timu zinazotaka mafanikio na pia kuweza kuuza wachezaji kwa timu kubwa hapa nchini au nje ya nchi kama zilivyo Simba na Yanga,” alisema Kim.
Alipoulizwa licha ya kiwango chao, iweje hakuna mchezaji wa City katika kikosi cha Taifa Stars, Kim alisema: “Tuliita wanne  kwenye Future Young Taifa Stars, lengo lilikuwa kuangalia uwezo wao, ukweli wana uwezo lakini wanakosa uzoefu, hivyo sikuweza kuwajumuisha kwenye timu iliyokwenda Kenya kwa kuwa tulikuwa tunapigana vita kuhakikisha tunarudi na chochote.

“Naamini awamu ijayo, kutakuwa na wachezaji wengi wa Mbeya City kutokana na jinsi wanavyocheza.”

Stars inakabiliwa na mchezo mgumu wa kirafiki uliopo kwenye kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), Machi 5 mwaka huu, kwa kuchuana na Namibia  mjini Windhoek.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic