February 26, 2014



Mabingwa wa Afrika, Al Ahly wamewasili jijini Dar es Salaam leo saa 12 alfajiri na kupokelewa na wenzao waliotanguliwa pamoja na maofisa wa Ubalozi wa Misri nchini.


Kikosi kizima cha Al Ahly kimewasili huku viongozi na wachezaji wakigoma kuzungumza na waandishi wa habari, badala yake wakisisitiza wamechoka na safari.

“Sio sasa, hatuwezi kuzungumza, tuna uchovu sana,” alisema mmoja wa viongozi.


Juhudi za waandishi kuwashawishi wazungumze zilikwama na muda mwingi waliutumia kuwasisitiza wachezaji waende kwenye basi lililoandikwa Kakore Trans kwa ajili ya kuondoka kwenda katika hoteli ya Kempinsky jijini Dar ambako ndiyo watafikia.







0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic