February 13, 2014


Kiungo Mtanzania, Mwinyi Kazimoto huenda akaweka rekodi kucheza Ligi Kuu Qatar iwapo timu yake itashinda mechi tatu zilizobaki.


Kazimoto anakipiga katika timu ya Al Markhiya inayoshiriki Ligi Daraja la Pili nchini Qatar na sasa katika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi hiyo.

Al Markhiya ina pointi 21 katika nafasi hiyo ya na iwapo itashinda mechi zake tatu zilizobaki basi itakuwa na uhakika wa kupanda ligi kubwa zaidi nchini humo.
KAZIMOTO AKIWA NA KIKOSI CHA AL MARKHIYA

Akizungumza kutoka Doha, Qatar, Kazimoto alisema wana hamu ya kupanda daraja na wamekuwa wakijitahidi kucheza kwa kujituma hadi walipofikia hapo wakiwa na mechi tatu.

“Ligi ni ngumu sana kwa kweli, kuna ushindani wa hali ya juu kuliko watu wanavyotegemea. Unajua timu za hapa zina uwezo kifedha hivyo zinasajili wachezaji kutoka Ulaya, mfano Hispania, Ureno na pia hata kutoka Brazil, Argentina, Chile na kwingine.
“Hali hiyo inasababisha kuwe na ushindani kuwa mkali sana, lakini tutajitahidi kadiri ya uwezo wetu na kama tukishinda mechi hizo tatu mambo yatakuwa uhakika,” alisema akionyesha kujiamini.
Kazimoto sasa amekuwa akiaminika katika kikosi hicho na ndiye amepewa ‘dimba la juu’ yaani namba nane na jukumu lake kubwa ni kuichezesha timu hiyo ambayo imekuwa na mabadiliko makubwa msimu huu.

Kiungo huyo aliyeanza kuchipukia akiwa na Ruvu Shooting, alijiunga na Al Markhiya akitokea Simba iliyoona kipaji chake na kumsajili na baada ya hapo aliendelea kufanya vizuri hadi alipojiunga na timu hiyo ya Qatar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic