February 14, 2014


Mabingwa wa Tanzania Yanga watacheza mechi yao ya marudiano na Al Ahly bila ya kuwa na mashabiki watakaoingia kutazama mechi hiyo.


Mechi hiyo itakayopigwa Machi 8 au 9 jijini Cairo haitakuwa na mashabiki isipokuwa wachache tu watakaopata kibali kutoka kwa Shirikisho la Soka la Misri (EFA).

Mwaka juzi zilizuka vurugu kubwa baada ya timu ya Al Masry kuwachapa vigogo Al Ahly kwa mabao 3-1, hali iliyosababisha watu 74 kupoteza maisha na wengine 1,000 kujeruhiwa wakiwemo wengine waliojeruhiwa vibaya sana. Baada ya hapo, mechi zinachezwa nchini humo, mashabiki wamekuwa hawaruhusiwi.

Mmoja wa maofisa wa EFA aliyejitambulisha kwa jina la Amir Mohammed aliliambia Championi Ijumaa juzi kuwa hakuna mashabiki watakaoruhusiwa kuingia uwanjani wakati wa mechi hiyo ya Ligi ya Mabingwa Afrika kutokana na sababu za kiusalama.
“Kawaida hata katika mechi za ligi watu wachache wenye kibali maalum wamekuwa wakiingia uwanjani, hakuna atakayeruhusiwa kuingia. Hivyo kama itakuwa ni Ahly na timu ya Tanzania, hakutakuwa na mashabiki.
“Labda wachache sana ambao tutawapa kibali, lakini kawaida ni viongozi na waandishi wa habari pekee. Zaidi ya hapo hatuwezi kuruhusu watu, waambie Yanga wanapaswa kulijua hilo,” alisema.
Ili kupata uhakika, gazeti hili liliamua kuwasiliana na baadhi ya Watanzania wanaoishi katika jiji la Cairo na mmoja wao aitwaye Mohamed Mdoe alisema kawaida mashabiki katika jiji hilo wamekuwa wakiangalia mechi za ligi kuu kupitia runinga.
“Hakuna anayekwenda uwanjani, unajua baada ya zile vurugu za mashabiki hadi watu wakafariki dunia, walifungiwa na tumeishazoea. Mechi tunaziangalia kupitia runinga tu hapa,” alisema Mdoe.

Kawaida mashabiki husafiri na timu zinapokwenda kucheza na wengi wa Yanga wangependa kwenda na timu yao jambo ambalo sasa linaonekana litakuwa gumu kutokana na adhabu hiyo wanayoitumikia Misri kutokana na vurugu hizo zilizosababisha hadi watu kupoteza maisha.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic