February 19, 2014


Kiungo wa Simba SC, Henry Joseph, amewasihi mashabiki wa timu hiyo kuwa wavumilivu licha ya matokeo mabaya waliyoyapata katika mechi zao za hivi karibuni kwenye Ligi Kuu Bara.


Simba iliyopo nafasi ya nne kwenye mzunguko wa lala-salama wa ligi kuu msimu huu, imepata matokeo mabaya katika mechi zake tatu mfululizo kwa kutoka sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar, kisha kufungwa na Mgambo JKT 1-0, kabla ya kutoka sare nyingine ya 1-1 na Mbeya City.

 Henry alisema kuwa anajua wazi kuwa mashabiki wanaumia kutokana na matokeo hayo lakini amewataka kuwa wavumilivu kwani wamekuwa wakijitahidi kuhakikisha wanapata matokeo mazuri lakini mwisho mambo huwa mabaya.

Alisema kuwa Simba bado ina nafasi ya kumaliza katika nafasi nzuri za juu na kwamba kwa sasa wamejipanga vya kutosha kuhakikisha wanashinda mechi zote zilizobaki ili kuwapa mashabiki kile wanachokitaka.


“Matokeo tunayopata ni sehemu ya mchezo, huwa tunapambana ili kupata matokeo mazuri kwani tunajua kuna mashabiki kibao nyuma yetu huwa wanataka kuona tunashinda, lakini bahati mbaya hutokea kinyume na matarajio yetu,” alisema Joseph.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic