February 24, 2014


Wanachama wa Yanga sasa watanufaika na mfumo mpya kwa kutumia kadi maalum za kutolea fedha maarufu kama ATM, kama kadi za uanachama.

Habari za uhakika kutoka Benki ya Posta zimeeleza kuwa, benki hiyo iko katika mchakato wa mwisho kuidhamini Yanga na moja ya kazi zake itakuwa hiyo.
“Unajua tumezungumza na uongozi wa Yanga, ikiwezekana mchakato huo pia tutafanya na viongozi wa Simba. Lakini wanachama wa Yanga sasa watatumia kadi za Benki ya Posta kama kadi za uanachama.
“Kila wiki watakuwa wanakatwa kiasi fulani cha fedha kulipia ada yao, kitakuwa cha chini sana na huenda mwanachama asisikie maumivu kabisa.
“Si unajua kwa mwaka wanalipa Sh 12,000. Kwa mwezi ni shilindi elfu moja. Sasa jiulize kwa wiki atakatwa shilingi ngapi? Huu utakuwa ni utaratibu mpya na wa aina yake.
“Kadi ya uanachama na mwanachama ataweza pia kuhifadhia fedha zake kama anavyofanya katika akaunti zake benki,” kilieleza chanzo hicho kutoka katika benchi hiyo.
Iwapo itaanza, mpango huo utakuwa wa kwanza na wa aina yake kwa klabu za Tanzania ambazo ulipaji wa ada za wanachama wake umekuwa wa kusuasua.
Yanga na Simba ndiyo klabu zenye mashabiki wengi zaidi katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati lakini zimekuwa zikiteketea na umaskini kwa kuwa hakuna ubunifu.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic