Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic
amekataa kwamba alilikimbia gari lake aina ya Toyota GX 110 na kupanda basi la
wachezaji.
SALEHJEMBE ilimshuhudia Logarusic
akiachana na gari hilo na kukwea basi la wachezaji ikiwa ni dakika chache baada
ya mechi dhidi ya JKT Ruvu kwisha, huku Simba ikiwa imelala kwa mabao 3-2.
Logarusic alisogea karibu na gari lake,
huku ikionekana kama mtu ambaye machale yamemcheza aliondoka na kupanda basi.
Wachezaji wa Simba pamoja nay eye,
walitoka uwanjani hapo kwa kusindikizwa na magari ya jezi la polisi.
“Kweli nilipanda basi, lakini sikuwa
ninakimbia. Hakukuwa na sababu ya kufanya hivyo.
“Nilitaka kujua ndani ya basi wachezaji
wangu wanaendeleaje na kama kila kitu kinakwenda vizuri,” alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment