Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic
amesema timu yake imepania kushinda mechi ya leo dhidi ya Ruvu JKT ili kuweka
mambo sawa, lakini akakiri ushindi wa bao 7-0 wa Yanga dhidi ya Ruvu Shooting
umewaongezea presha.
Simba inashuka dimbani leo Taifa kuivaa
JKT inayoongozwa na kocha msaidizi wa zamani wa Yanga, Fred Felix Minziro ‘Majeshi’
au Baba Isaya.
Logarusic amesema leo lazima washinde
katika mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa, Dar ili kufanya
mambo yaende katika mwendo mzuri.
“Najua wengi watataka tuone tunashinda
mabao mengi zaidi, lakini kikubwa kwetu cha kwanza kitakuwa ni pointi tatu.
“Kama litafuata suala la mabao mengi,
basi hilo pia ni muhimu sana kwetu. Lakini pointi tatu tutazipa kipaumbele,”
alisema.
Logarusic alikuwa katika uwanjani wakati
Yanga ikiibutua Ruvu Shooting kwa mabao 7-0 katika mechi iliyopigwa kwenye
Uwanja wa Taifa jijini Dar, jana.
0 COMMENTS:
Post a Comment