Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm
amesema ikiwezekana kushinda mabao mengine saba, litakuwa jambo zuri.
Yanga iliweka rekodi mpya ya mabao
katika Ligi Kuu Bara msimu huu baada ya jana kuibutua Ruvu Shooting kwa mabao
7-0 katika mechi ya Ligi Kuu Bara, jana.
Mholanzi huyo amesema anapenda kuona
kikosi chake kinashinda mabao mengi zaidi.
Lakini akasisitiza, kama litatokea suala
la kushinda mabao saba litakuwa safi zaidi.
“Ikiwezekana itakuwa vizuri zaidi,
ikishindikana basi ushindi ni jambo zuri zaidi hata kama ni mabao mawili,”
alisema.
Kocha huyo aliyefanya kazi nchini Ghana
kwa mafanikio, amesisitiza kikosi chake kitaendelea kufanya vizuri zaidi.
0 COMMENTS:
Post a Comment