February 22, 2014

LOGARUSIC ATOA MBINU ZA KUREKEBISHA MWENDO
Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amesema moja ya njia ya kufanya vema kwa kikosi chake ni wachezaji wake kukataa makosa zaidi.

Kocha huyo raia wa Croatia amesema makosa makubwa wanayoyafanya ndiyo yamekuwa yakiwa mwelekeo mbaya katika ligi hiyo.

“Kukosea mkaruhusu mkafungwa au kukosea mkakubali kupoteza nafasi ya kufunga, tayari hilo ni kosa na mnakuwa mmejiondoa njiani.
“Kama unapata nafasi unatumia, au walinzi hawatoi nafasi ya timu pinzani kufunga, basi njia ya kufanya vizuri ni lahisi kabisa.
“Wachezaji wangu ninazungumza nao sana, lakini najua ni suala la kurudia na kurudia tena ili watu waelewe.
“Tumezunguka mikoani na kuambulia pointi mbili tu, si sahihi na lazima tukatae kwamba huo si mwendo mzuri unaotufaa sisi,” alisema.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic