February 22, 2014



Kocha Mkuu wa Ruvu JKT, Fred Felix Minziro amesema kupoteza mechi kwa mabao 6-0 dhidi ya Prisons haina maana watakuwa laini dhidi ya Simba.

Kikosi cha Minziro kinakutana na Simba kesho baada ya siku chache kupokea kipigo cha mabao 6-0 dhidi ya Prisons ya Mbeya.
Minziro aliyekuwa kocha msaidizi Yanga kabla ya kurejea JKT amesema kila mchezo unajitegemea na lengo lao ni kufanya vizuri pia kujifunza kupitia makosa.
“Tunachotaka ni kufanya vizuri, wachezaji wanajua tumepoteza na kuna makosa tulifanya. Hivyo hatupaswi kupoteza tena.
“Tunatakiwa kurekebisha mambo wakati tunakutana na Simba, tumejiandaa na tunaendelea kujiandaa. Watu wasidhani itakuwa mechi lahisi,” alisema Minziro.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic