February 22, 2014


Wayne Rooney noma, sasa amesaini mkataba mpya na Manchester United ambao utambakiza katika klabu hiyo hadi mwaka 2019.

Mkataba huo pia umevunja rekodi kwa kuwa moja ya mikataba ghali zaidi kwa kuwa atakuwa akilamba pauni 300,000 (Sh milioni 750), kwa wiki huku kimuacha Sergio Aguero anayechukua pauni 200,000 kwa wiki pia.
Rooney kusaini mkataba huo mpya ni sawa na ushindi kwa Kocha David Moyes ambaye, jana amesema klabu hiyo haijawahi kuwa na mpango wa kumuuza Rooney.


Chelsea walifikia kutoa hadi pauni milioni 30 mwishoni mwa msimu uliopita wakimtaka Rooney baada ya taarifa kuzagaa hakuwa akielewana tena na kocha aliyepita, Alex Ferguson.

Katika mkataba huu mpya, kuna kipendegelea cha Rooney maarufu kama Wazza kuwa balozi wa Manchester United, mara tu atakapostaafu soka.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic