February 23, 2014

 
RAIS WA TFF, JAMAL MALINZI

WAHUSIKA katika masuala ya ufundi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ndiyo wanaokaa na kupanga ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Namna ya ligi inavyochezwa ni nyumbani na ugenini, lakini mambo yanakwenda hivi; mechi zinachezwa kwa mizunguko miwili. Nyumbani na ugenini.
Mfumo huo ni duniani kote, lakini hapa nyumbani inakuwa hivi, kama katika mzunguko wa kwanza Simba ilianza na Ruvu Shooting, basi katikat mzunguko wa pili, vivyo hivyo itaanza tena na timu hiyo. Sidhani kama ni sahihi sana, ingawa si vibaya.
Lakini katika upangaji ratiba kuna umuhimu wa kuangalia mechi za kimataifa, kuwapa nafasi wawakilishi wan chi ambao wanashiriki michuano ya kimataifa. Kwa hapa nyumbani tumebakiza timu moja tu ambayo ni Yanga.
Ukiangalia ratiba ya Ligi Kuu Bara, unaweza kudhani inaishambulia Yanga ili isifanye vizuri katika michuano ya kimataifa. Lakini ninaamini haikuwa na nia mbaya, lengo ni kufanya mambo yaende kwa utaratibu.
Pamoja na kutaka mambo yaende safi, lakini inaonekana wanaopanga wamekuwa hawafikirii namna ambavyo wanaweza kuzisaidia timu za nyumbani zinazoshiriki michuano ya kimataifa. Huenda Yanga wanaona sahihi, lakini nina haki ya kukosoa au kuchangia ninapoona si sawa.
Yanga itashuka kuivaa Al Ahly ya Misri kati ya Machi Mosi au Machi 2, hiyo itakuwa ni Jumamosi au Jumapili ijayo. Kumbuka watakuwa na mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya wapinzani wao wakubwa baada ya Simba na Azam FC, Prisons pia wana ushindani wa juu.

Mechi ya Yanga dhidi ya Prisons ni kati ya big match katika soka hapa nyumbani. Kama Yanga itacheza Jumamosi dhidi ya Al Ahly, maana yake itakuwa imepumzika mbili tu baada ya kucheza na Prisons halafu itawavaa wababe hao wa Afrika, si kitu cha kawaida.

Bado itakuwa hivi, kama Yanga itacheza Jumamosi, maana yake ndani ya siku nne, itakuwa imecheza big match mbili. Nafikiri bado si sahihi kwa maana ya mwendo wa timu zetu, ninaamini Yanga wanaweza kujitutumua, jambo ambalo ni nzuri lakini ratiba lazima ziwe na ufundi wa kuzisaidia timu zinazoliwakilisha taifa katika michuano ya kimataifa.

Angalia Al Ahly mechi yao ya mwisho ilikuwa ni jana dhidi ya Misr Lel Makasa na baada ya hapo watakuwa na siku tano bila mechi na utaona timu waliyopangiwa ingawa watapumzika siku hiyo. 
Hii inawapa funzo wataalamu wa TFF, kwamba baada ya mechi dhidi ya Ruvu Shooting, Yanga ingepewa nafasi ijiandae.
Kuaicha icheze tena katikati ya wiki, bila kuangalia suala la majeruhi, uchovu na tena wanapokuwa na mechi ngumu au kubwa dhidi ya timu kama Prisons, ni kuwaingiza Yanga kwenye dimbwi la hofu au dalili za kutofanya vizuri.

Hapa inaonyesha namna ambavyo watalaamu wa Shirikisho la Soka la Misri (Efa) wanavyojua umuhimu wa timu inayoliwakilisha taifa lao katika michuano ya kimataifa. Hili hata wale wa TFF wanapaswa kujifunza.
Wataalamu hao wa Efa wanaipa Al Ahly siku moja ya kusafiri na si siku nzima, maana si zaidi ya saa 5 kutoka Cairo hadi Dar. Lakini wameonyesha wanaelewa wanajua umuhimu na ugumu pia wa mechi dhidi ya timu inayotoka kwenye taifa lingine. Kumbuka ni ligi ya mabingwa, wanaokutana ni mabingwa wa nchi mbalimbali.

Lakini TFF walipaswa kujua Yanga inakutana na Al Ahly ambao ni mabingwa wa Afrika, au wangeweza kuweka tahadhari mapema, hapa lengo si ushabiki au kumfurahisha nani. Badala yake ni utaifa kwa kuwa tu Yanga wanaiwakilisha Tanzania, nchi yetu ambayo ndiyo kwetu.

Hivyo, TFF wanaweza kushiriki kuwasaidia Yanga kufanya vizuri, ratiba inayowapa nafasi ya kujiandaa vizuri ni sehemu ya kuonyesha utaifa. Pia hii isingefaa kwa Yanga tu, badala yake kila timu itakayopata nafasi ya kuliwakilisha taifa katika michuano ya kimataifa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic