February 12, 2014

MARSH AKIZUNGUMZA NA ABDUL MOHAMMED WA BBC

Hali ya Kocha Msaidizi wa timu  ya taifa (Taifa Stars), Sylvestre Marsh, inaendelea vizuri baada ya kuchukuliwa vipimo kwa mara ya pili juzi Jumatatu ambapo majibu ya vipimo hivyo bado hayajulikani lini yatakuwa tayari.


Kocha huyo ameanza kuugua hivi karibuni  ikiwa ni wiki ya pili sasa tangu alazwe katika Hospitali ya Taifa  ya Muhimbili ambako amekuwa akifanyiwa uchuguzi ili kubaini tatizo linalomsumbua.

Akizungumza na Championi Jumatano, kocha huyo alisema kwa sasa anaendelea vizuri, japokuwa bado anaendelea na vipimo.
Marsh alisema kwa kiasi fulani anaendelea vizuri, japo baada majibu ya vipimo kutoka ndipo ataanza kupata matibabu zaidi kufuatia madaktari kugundua tatizo lake.

“Nimepata vipimo siku ya leo lakini sijajua majibu yatatoka lini, hii ni kutokana na aina ya vipimo nilivyofanyiwa huwa inachukua muda mrefu majibu kutoka, kwa hiyo nitaendelea kuwa hapa hospitalini mpaka pale nitakapopata majibu.

“Lakini  kwa majibu ambayo siyo rasmi,  inasemekana kuwa huenda nikawa na uvimbe katika sehemu ya kifua ambayo chakula hupita, japo siyo majibu ya vipimo niliyopewa. Majibu yakiwa tayari nadhani ndiyo tutajua ni tatizo gani.

“Zaidi sana nawashukuru wale wanaojitoa kuja kunijulia hali hapa hospitalini, Mungu awatie  nguvu na wasichoke. Ninaamini nitapona tu nikiendelea kupata matibabu vizuri,” alisema.


 SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic