February 12, 2014


Timu ya Ferroviario de Beira ya Msumbiji imekubali kazi iliyofanywa na wachezaji wawili wa Azam, Kipre Tchetche na Salum Aboubakar ‘Sure Boy’.


Azam ilikuwa mwenyeji wa Ferroviario kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika uliopigwa juzi kwenye Uwanja wa Chamazi.

Kocha Msaidizi wa Ferroviario, Victor Martin, alisema  katika mechi hiyo hakukuwa na mchezaji aliyeonekana uwanjani zaidi ya Tchetche na Sureboy huku akisisitiza kuwatafutia mbinu mbadala kwa ajili ya kuwadhibiti watakaporudiana nao baada ya wiki moja jijini Maputo, Msumbiji.

 “Yaani kuna yule aliyefunga bao (Tchetche) na aliyevaa kitambaa cha unahodha (Sure Boy), walikuwa wanacheza vizuri sana, ni wachezaji hatari wanaohitaji ulinzi wa kutosha uwanjani lakini nafikiri tutakaporudiana nao tutakuwa tayari tumeshapata dawa ya kuwazuia, kwa kweli ni aina ya wachezaji ninaotamani hata siku moja tuwe nao kikosini,” alisema Martin.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic