February 15, 2014

 
SOKOINE ITAKAVYOONEKANA SAA CHACHE ZIJAZO
Hali ya jiji la Mbeya lineonakana kuchangamka huku kila sehemu ya mji huo gumzo likiwa ni mechi ya Ligi Kuu Bara kati ya wenyeji Mbeya City dhidi ya Simba.


Mashabiki wengi wanaonekana mitaani wakiwa na jezi za rangi ya zambarau na nyeupe ambayo huvaliwa na Mbeya City na wachache tu, tena wengi ni wale waliosafiri na timu hiyo kutoka jijini Dar nao wamepiga uzi mwekundu na weupe.
MASHABIKI SIMBA WATAKUWEPO KUISHANGILIA TIMU YAO

Lakini mashabiki wa Mbeya City wanaonekana kujiamini zaidi kwa kuwa timu yao hiyo haijawahi kufungwa kwenye Uwanja wa Sokoine tokea ligi inaza na imepoteza mechi moja tu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar dhidi ya Mabingwa Yanga.

Lakini Simba wamekuwa wakisisitiza leo ni siku ya kuinyamazisha Mbeya kwa kuwafunga wenyeji wao hao kwa mara ya kwanza tokea kuanza kwa ligi hiyo, kiti ambacho Kocha Juma Mwambusi wa Mbeya City amesema ni nadra kutokea.

Katika mechi ya kwanza jijini Dar, timu hizo zilimaliza mechi kwa sare ya bao 2-2, Mbeya City wakisawazisha mabao yote baada ya kuwa nyuma kwa mabao mawili. Je, leo itakuwaje? Vuta subira.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic