February 15, 2014



Ahadi ya kuwa Mbeya City itaitwanga Simba leo kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya imeshindwa kutimia baada ya timu hizo kumaliza dakika 90 kwa sare ya bao 1-1.

Katika mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara iliyopigwa kwenye Uwanja huo, Mbeya City ndiyo ilikuwa ya kwanza kuandika bao kwa mkwaju wa penalti baada ya beki William Galas wa Simba kuunawa mpira.

Bao hilo likadumu hadi mapumziko lakini kipindi cha pili Simba wakaonekana kupata uhai zaidi na kufanikiwa kupata bao lililofungwa na Amissi Tambwe.
Pamoja na mashambulizi ya zamu, lakini ilionekana Simba walikuwa wameimarika zaidi katika kipindi hicho baada ya kubanwa sana katika kipindi cha kwanza.
Kama wangekuwa makini wangeweza kupata  bao la ushindi, lakini mwisho mechi hiyo iliyoingiza mashabiki wengi sana ilimalizika kwa sare hiyo.
Awali, Mbeya City walikuwa wametamba kuimaliza Simba ambayo katika mechi ya kwanza jijini Dar walitoka nayo sare ya mabao 2-2 wenyewe wakitoka nyuma kwa mabao mawilia na kusawazisha yote.
Katika michezo yake mitatu iliyopita ukiwemo huo wa leo, Simba imepoteza mmoja na kutoka sare miwili.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic