February 22, 2014

Kocha Msaidizi wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa ameingia Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wakati Yanga ikikipiga na timu yake ya zamani ya Ruvu Shooting na kushangiliwa kwa nguvu na mashabiki.

Mashabiki hao wameripuka kwa furaha baada ya Mkwasa kuingia uwanjani katika dakika ya 17 wakati mechi hiyo inaendelea.
Mkwasa alikuwa nchini Misri alikokwenda kuisoma Al Ahly iliyokuwa inacheza dhidi ya CS Sfaxien katika mechi ya Kombe la Super Cup na kushinda kwa mabao 3-2.
Mara tu baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Mkwasa alipitiliza moja kwa moja hadi Uwanja wa Taifa.

Yanga itaivaa Al Ahly katika mechi mechi itakayoigwa Jumamosi ijayo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic