February 10, 2014

HUYU MAMA MUUZA MIHOGO YEYE ALIKABIDHIWA TIMU YA WAHARIRI WA CHAMPIONI

Na Lucy Mgina
IMETIMIA! Ile siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na wasomaji wa Gazeti la Championi kujinyakulia shilingi milioni 10 taslimu, sasa imetimia kwani leo kwenye Viwanja vya Mbagala Zakhem jijini Dar ndiyo itafanyika droo hiyo ya mwisho.


Hii ni droo ya mwisho ambapo awali katika droo zilizopita walipatikana washindi mbalimbali wa sofa seti, friji, flat screen na dekoda yake, dinner seti na nyinginezo kibao.

Meneja wa Global Publishers Ltd ambao ni wachapishaji wa gazeti hilo, Abdallah Mrisho, alisema ni wakati wa mavuno kwa wasomaji wake ambao walituma kuponi ili kujishindia kitita hicho.

Alisema kila kitu kipo tayari kwani leo pia watatoa jezi na zawadi nyingine kibao kutoka kwa Mr Championi kabla ya mshindi mkubwa kukabidhiwa chake mapema.

Alisema kwa ambao hawajakabidhi kuponi wazilete mapema leo Jumatatu kadiri wawezavyo kwani hakuna kiwango maalum.

Alizitaja sehemu ambazo unaweza kuziwahisha kuponi kwa wakazi wa Dar kuwa ni Dar Live Mbagala, Ubungo Terminal, Magomeni Mwembechai, Mwenge, Kariakoo kwenye ‘round about’,  Zahor Matelephone iliyopo Kariakoo, Buguruni, Ofisi za Global, Mwenge, Tegeta Kona ya Nyuki, Ubungo Yenu Bar na Kigamboni Feri.
“Ambao bado hawajaleta kuponi zao wafanye haraka leo asubuhi na mapema wazilete kwani mchana tutakuwa na droo yenyewe ambayo mshindi atajinyakulia shilingi milioni 10.
“Wasomaji watambue hii ni droo kubwa ambayo mshindi atapatikana kwa uwazi na itachezeshwa mbele yao, hivyo hawatakiwi kuwa na hofu,” alisema Mrisho.

Droo hiyo itasimamiwa na ofisa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania (Gaming Board), Emmanuel Ndaki.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic