February 10, 2014


Uongozi wa Klabu ya Simba umesema kuwa, upo tayari kukaa mezani na TP Mazembe kumuuza kiungo mshambuliaji, Ramadhani Singano ‘Messi’ kwa dau zaidi ya lile alilouzwa mshambuliaji Emmanuel Okwi katika Klabu ya Etoel du Sahel ya Tunisia.


Simba ilimuuza Okwi kwa dola 300,000 ambazo ni zaidi ya Sh milioni 480 kwenye kikosi cha Etoile du Sahel, lakini mpaka leo haijapata fedha yoyote kutokana na mauzo hayo.

Hivi karibuni uongozi wa TP Mazembe ya Lubumbashi, DR Congo ilimtuma kiongozi wa usajili wa timu hiyo ambaye aliangalia mechi kati ya Simba na Rhino ya Tabora kwa ajili ya kumfuatilia Messi kufuatia kupata taarifa kuwa yupo fiti.

Ezekiel Kamwaga, alisema iwapo Mazembe itakuwa inamhitaji mchezaji huyo, wapo tayari kukaa meza moja na kuzungumza ili biashara ifanyike, kwani hawawezi kumzuia mchezaji yeyote yule iwapo atapata dili nje na dau lake ni zaidi ya alilouzwa Okwi.

“Kama kuna klabu inamhitaji Messi ije Simba ili tuweze kuzungumza na tuweze kuangalia maslahi yetu na ya mchezaji kiujumla.


“Dau la Messi ni tofauti na lile tulilomuuzia Okwi la dola 300,000. Mauzo ya Messi yatakuwa ya juu zaidi kulingana na ubora wa mchezaji, pia kwa kuwa anatarajia kuwa katika mpira kwa muda mrefu zaidi tofauti na ilivyo kwa Okwi,” alisema Kamwaga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic