February 15, 2014


Wakati mechi kati ya Mbeya City dhidi ya Simba inatarajia kuanza saa 10:30, vurugu kati ya makomandoo wa timu hizo wamepambana kwa kuzichapa vibaya.


Makomandoo hao wamezichapa mara baada ya wachezaji wa Simba kuingia uwanjani na kukatiza katikati ya uwanja huku ikiwa ni dakika 5 baada ya basi lao kuingia uwanjani likiwa tupu.

Wakati basi linaingia uwanjani, mashabiki wa Mbeya City waliojazana kwa wingi uwanjani hapo walilizomea wakidhani lina wachezaji hao, lakini kumbe lilikuwa tupu.

Dakika tano baadaye huku maswali yakiwa yamejaa uwanjani hapo, wachezaji wa Simba walianza kuingia wakitembea taratibu na kukatiza katikati ya uwanjani hali iliyosababisha kuzuka kwa tafrani hilo na mwisho, polisi wakaingilia na kuamua ugomvi na wachezaji wa Simba waliokuwa wakishuhudia ugomvi huo kama muvi, wakaingia vyumbani.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic