February 17, 2014



Pamoja na kufungwa mabao 2-0 na Ferreviario ya Msumbuji na kutolewa kwa jumla ya mabao 2-1, wachezaji wa Azam FC leo wamerejea jijini Dar wakiwa na furaha tele.

Wachezaji hao, hasa wale wa kigeni walionekana na furaha ambayo haikupishana na ile ya Yanga ambao walifanikiwa kusonga mbele kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuichapa Komoronize kwao Moroni kwa mabao 5-2 na kukamilisha idadi ya mabao 12-2.
Hata kama wangekuwa na furaha, bado wachezaji wa Azam FC walipaswa kuonyesha maumivu yao na hasa kwa kuwa wakati wanashiriki mara ya tatu michuano hiyo, safari ya tatu ndiyo wametolewa mapema zaidi.
Angalau kidogo baadhi ya wachezaji hasa wale wazalendo walionyesha kutokuwa na nyuso za furaha, hali inayoweza kuonyesha hawakufurahishwa na kuishia hapo.













0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic