February 27, 2014


Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) liko katika hatua ya mwisho kumtangaza kocha mpya na inaelezwa atakuwa ni raia wa kati ya nchini mbili, Ujerumani au Uholanzi.

Tayari TFF imemtupia virago Kocha Kim Poulsen ingawa imekuwa ikielezwa kuwa imefanya hivyo kwa kukubaliana naye kamba wavunje mkataba.

TFF chini ya Malinzi ilionekana kutoridishwa na kasi ya Poulsen tokea ilipoingia madarakani.

Fununu za yeye kupoteza kazi zikaenea lakini bado maofisa wa TFF wakawa ‘wanafunika kombe’ kiana.

Lakini leo, rasmi TFF imetangaza kumalizana na Mdenishi huyo ambaye alichukua nafasi hiyo kutoka kwa Mdenishi mwingine, Jan Poulsen.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic