February 14, 2014


Winga mwenye kasi wa Ashanti United, Said Maulid ‘SMG’, amekumbwa na tatizo jipya la kuugua kila inapokaribia mechi ya Ligi Kuu Bara.


Tangu kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi hiyo, SMG hajacheza mechi yoyote ambapo Ashanti imecheza mechi tatu.

Awali alikuwa akisumbuliwa na goti lakini baadaye akapona akajiunga na wenzake kwa ajili ya maandalizi ya mzunguko wa pili, siku chache kabla ya kuanza kwa ligi akajitonesha na hali hiyo imekuwa ikijirudia mara kadhaa zinapokaribia mechi.

Kocha Mkuu wa Ashanti, Abdallah Kibadeni amesema SMG anakuwa mzima wakati wa mazoezi lakini mechi zinapokaribia lazima ajitoneshe.

“Unaweza kumuona mzima siku zote na anafanya mazoezi lakini zinapobaki siku chache kabla ya mechi, anajitonesha au anaumia.

“Angekuwa ni kijana mdogo ningesema anaogopa mechi lakini huyu SMG ni mtu mzima, naamini hawezi kuniongopea, hii ni dalili ya mtu kuelewa anachokifanya, kama angekuwa ana tamaa angetaka kucheza hivyohivyo,” alisema Kibadeni.

Kesho Jumamosi, Ashanti itavaana na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Chamazi, Kibadeni anasema kama SMG akiendelea kuwa fiti anaweza kumtumia kwenye mechi hiyo. 


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic