February 14, 2014



Simba imetamba kwamba itatibua rekodi ya Mbeya City kutofungwa hata mechi moja kwenye Uwanja wake wa nyumbani wa Sokoine.


Kikosi cha Simba ambacho kipo Mbeya, kesho kina kazi ya kupambana na Mbeya City kwenye uwanja huo na katika mechi ya mzunguko wa kwanza, zilitoka sare ya mabao 2-2 kwenye Uwanja wa Taifa, City wakisawazisha zote mbili.

Katika Ligi Kuu Bara, Mbeya City iliyo katika nafasi ya tatu, imepoteza mechi moja tu na yenyewe ni ugenini dhidi ya Yanga.

Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola amesema wamepania kushinda na wanajiandaa vilivyo kuhakikisha wanashinda mechi hiyo.
“Tunaweza kuvunja hiyo rekodi, huu ni mpira na hata kama wanajiamini na sisi tunajiamini na tunachotaka ni ushindi,” alisema.
“Wachezaji wote wako safi na tumejiandaa, tunachosubiri ni muda wa kuingia uwanjani na kufanya kazi yetu,” aliongeza nahodha huyo wa zamani wa Simba.

Simba imekuwa ikisuasua, kwani katika mechi mbili za mwisho za Ligi Kuu Bara imetoka sare dhidi ya Mtibwa Sugar na kuchapwa 1-0 na Mgambo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic