February 14, 2014


Kikosi cha Yanga kipo kamilini ugenini Moroni nchini Comoro kuwamaliza wenyeji wao Komorozine.

Katika mechi hiyo ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika inayosubiriwa kwa hamu mjini humo, Yanga imesisitiza ipo kamili.
Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu amesema amepewa taarifa kwamba kesho watafanya kila linalowezekana kuibuka na ushindi.
YANGA TAYARI WAKO COMORO KWA AJILI YA MECHI YA KESHO

“Hata kama katika mechi ya kwanza tulishinda kwa mabao saba bila, lakini bado tunahitaji ushindi na wachezaji wanalijua hilo.
“Nimeambiwa kikosi kipo fiti na tutafanya kila linalowezekana kuhakikisha tunashinda,” alisema.
Yanga iliitwanga Komorozine bao 7-0 katika mechi ya kwanza kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar na sasa inahitaji sare ya aina yoyote au hata ikipoteza 6-0 bado itasonga mbele.

Baada ya hapo, Yanga ikisonga mbele itakutana na mabingwa wa Afrika, Al Ahly na mechi itaanza kupigwa jijini Dar Machi Mosi kabla ya kurudiana wiki moja baadaye.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic