Zikiwa zimebaki mechi saba ili Ligi Kuu
ya Tanzania Bara imalizike, mshambuliaji wa Simba, Amissi Tambwe, ameshafikisha
idadi ya mabao yaliyofungwa na Kipre Tchetche, msimu uliopita.
Kipre, msimu uliopita alikuwa mfungaji
bora baada ya kufunga mabao 17 kwenye ligi kuu, lakini mabao mawili ambayo
Tambwe alifunga jana yameshamfanya afikie idadi hiyo.
Hii ni rekodi mpya inawekwa na
mshambuliaji huyo raia wa Burundi ya kufikia idadi ya mfungaji bora wa msimu
uliopita zikiwa zimebaki mechi nyingi.
Kipre msimu huu hayupo kwenye kiwango
kizuri hali ambayo imekuwa ikimpa nafasi kubwa Tambwe ya kuwika kwenye mbio za
ufungaji bora.
Nyuma ya Tambwe ambaye huu ndiyo msimu
wake wa kwanza, yupo Kipre mwenye mabao 10 na Elias Maguli tisa, hali ambayo
inaonyesha ni vigumu kumkuta kinara huyo.
Tambwe anashikilia rekodi nyingine ya
kufunga mabao matatu hat trick mbili kwenye michezo miwili ya ligi hiyo msimu
huu na inaonekana kuwa anaweza kufunga mabao mengi zaidi na kuweka rekodi
nyingine kuanzia ligi imeanza kuchezwa na timu 14.
0 COMMENTS:
Post a Comment