February 26, 2014


Na Saleh Ally
Mabingwa wa soka Tanzania, Yanga wamelazimika kumwaga kitita cha dola 10,000 (zaidi ya Sh milioni 16) kuwapa Al Ahly kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Jumamosi.


Timu hizo zitapambana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na tayari mabingwa hao wa Afrika wametua nchini, tayari kupambana na mabingwa hao wa Tanzania waliopania kuuangusha mbuyu huo.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Yanga chini ya Mwenyekiti Yusuf Manji na naibu wake, Clement Sanga zinaeleza kwamba, uongozi wa Yanga umeukabidhi ule wa Al Ahly fedha hizo kwa ajili ya matumizi yao watakapokuwa nchini kwa kuwa walikataa hoteli waliyopangiwa.

“Yanga ilitumia kiasi hicho cha fedha kuwalipia hoteli Komorozine ya Comoro ilipokuwa nchini, sasa Ahly wakaikataa hoteli wakitaka wapangiwe Kempinsky, kitu ambacho kingekuwa ni gharama kubwa sana na Yanga ikakataa.

“Kwa kuwa ilitenga hiyo dola elfu kumi, basi ikawakabidhi Al Ahly na wenyewe ndiyo wameongezea na kwenda kupanga katika hoteli wanayoitaka. Hivyo Yanga nayo inaweza kulipwa fedha au kupewa hoteli ya kiwango hicho itakapokwenda Cairo,” kilieleza chanzo hicho cha uhakika.


Tayari watu wawili wametangulizwa nchini kufanya maandalizi ya mechi hiyo dhidi ya Yanga na juzi na jana walikuwa kwenye hoteli hiyo ya Kempinski kuweka mambo sawa pamoja na Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Kimataifa ya Tanganyika (IST) tawi la Upanga jijini Dar es Salaam kuhakikisha wanafanya mazoezi kwenye uwanja wenye kiwango wanachoamini ni bora.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic