March 2, 2014


Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo (Taswa) kimefanya uchaguzi wake jana kwenye Ukumbi wa Water Fronti na kupata viongozi wapya.


Akizungumza kabla ya kutangaza matokeo hayo Katibu Mkuu wa Kamati ya Uchaguzi wa Taswa Mwina Kaduguda alisema anawapongeza waandishi wa habari kwa kutimiza wajibu wao kwa kuchagua viongozi hao.
“Niwapongeze wote ambao mpaka sasa mpo humu ndani, najua katika uchaguzi wowote lazima kutatokea matatizo ya hapa na pale, lakini wajumbe mmetumia demokrasia yenu,” alisema.
Pia Kaduguda alitoa somo kwa viongozi ambao wameshinda kuhakikisha wanatimiza na kuyafanya yale ambayo waliwahaidi wapiga kura kabla ya kuwachagua.
Kaduguda ambaye aliwahi kuwa Katibu Mkuu klabu ya Simba aliwataja kwa upande walioshinda nafasi ya wajumbe wa Taswa Hassan Bumbuli, Ibrahim Bakari, Mroki Mroki, Musa Juma, Chacha Maginga, Rehule Nyaulawa na Mwani Nyagasa.
Nafasi ya Mhazini Msaidizi ilichukuliwa na Zena Chande aliyemsindia mpinzani wake Elius Kambili, huku Mhazini Mkuu ikichukuliwa na Shija Richard aliyemshinda Mohamed Mkangara.
Kwa upande wa Katibu Msaidizi aliyeshinda ni Grace Hoka, huku nafasi ya Katibu Mkuu ikichukuliwa na Amiri Mhando ambaye alikuwa akitetea nafasi hiyo na alipigiwa kura za ndio na hapana  kutokana na kugombea nafasi hiyo peke yake na kushinda kwa kishindo.
Kwa upande wa Mwenyekiti Juma Pinto amerejea tena madarakani kwa kupigiwa kura za ndio na hapana baada ya nafasi hiyo mgombea akiwa pekee.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic