April 2, 2014


Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm,  juzi alipandwa na hasira nusura amchape makonde beki wake, Kelvin Yondani.


Yanga ilivaana na Mgambo JKT kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara uliopigwa katika Uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga na kula kichapo cha mabao 2-1.

Tukio hilo lilitokea mara baada ya mchezo kumalizika  ambapo Pluijm alimfuata Yondani aliyekuwa amesimama na kuanza kumlalamikia kwa madai kuwa beki huyo alifanya kosa kusababisha penalti iliyozaa bao la pili kwa Yanga.


Wakati kocha huyo alionekana kukasirika huku akiongea kwa ukali, Yondani alionyesha hali ya kutojali na kutaka kuondoka kwenda kwenye gari lakini Pluijm alimvuta mkono kwa nguvu na kuendelea kumpa dozi ya maneno.


Hata hivyo, waandishi waliokuwa wanamsubiri kocha huyo ili awape tathimini ya mchezo ndiyo waliomuokoa Yondani baada ya kumvuta mwalimu huyo ili wafanye naye mahojiano na Yondani ambaye hakujibu kitu na kuingia moja kwa moja kwenye basi la wachezaji wa timu hiyo lililokuwa karibu naye.

“Lile tukio la pale uwanjani si uliliona jinsi kocha alivyokuwa akimfokea Yondani? Hali haikuishia hapo, kocha alipanda tena kwenye basi na kwenda mpaka alipokaa Yondani na kuendelea kumpa dozi.

“Kweli kocha alikuwa amekasirika sana, nafikiri Yondani alifanya vizuri kutomjibu kama angemjibu labda angempiga hata makofi,” kilisema chanzo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic