April 23, 2014


Kocha Zdravko Logarusic amesema anaamini atabaki Simba kama wao watakuwa tayari kufanya hivyo.

Lakini akasisitiza, iwapo ataondoka nchini keshokutwa Ijumaa, basi anaweza kuendelea na kusaka maslahi mbele kwa mbele.
Akizungumza na SALEHJEMBE, Loga alisema anaona ni vizuri kuwapa nafasi Simba ambao ni waajiri wake.
“Nikiona hawana mpango, basi nitaangalia kazi kwingine. Unajua vizuri kutoa nafasi kwa mwajiri wako kwanza.
“Halafu utaona anakuhitaji au la, ikiwa anakuhitaji, basi utajua. Kama hakuhitaji pia utajua,” alisema Loga.

Loga anatarajia kuondoka nchini Ijumaa kurejea kwao Croatia ikiwa ni baada ya msimu kumalizika.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic