April 16, 2014



Na Saleh Ally
ATLETICO Madrid ndiyo vinara wa Ligi Kuu ya Hispania La Liga, haijawahi kutokea kwa kipindi cha zaidi ya misimu nane timu nyingine kuwa katikati au juu ya Real Madrid na Barcelona.

Kila timu imebakiza mechi tano kumaliza La Liga na Atletico wana pointi 82 kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikifuatiwa na magwiji Real Madrid wenye pointi 79 na Barcelona wenye 78.

Pamoja na kuaminika Real Madrid na Barcelona ni lazima ziwe mabingwa kutokana na historia ya ligi hiyo, lakini inawezekana kabisa Atletico kuwa mabingwa wa La Liga msimu huu. Sababu ziko nyingi.

Pia imezitambia Madrid na Barcelona kila walipokutana. Kuwa kileleni kwa Atletico si la kubahatisha kwa kuwa timu hiyo kutoka jijini Madrid imefika hapo kwa ubora ambao unaonekana wazi.
Takwimu:
Kitakwimu Atletico imeshinda mechi 26 ambazo ni nyingi zaidi kuliko Real Madrid na Barcelona ambazo kila moja imeshinda 25.
Atletico Madrid imepoteza mechi tatu ambazo ni chache zaidi kuliko zile walizopoteza Madrid ambazo ni nne na Barcelona tano.
Mechi nane:
Ukiangalia mechi nane za mwisho za La Liga kwa kila timu kati ya hizo tatu, Atletico Madrid bado inaonekana kuwa bora kuliko wakongwe hao wa Hispania.

Katika mechi nane za mwisho, Atletico imeshinda saba na sare moja tu ambayo ndiyo rekodi nzuri na ya juu katika kipindi hiki kwenye La Liga. Ubora wao umepanda kwa asilimia 31.
Madrid wao katika mechi hizo nane za mwisho, wameshinda tano, wamepoteza mbili na sare moja na ubora wao umeshuka kwa asilimia 28.

Kwa upande wa Barcelona katika mechi nane za mwisho, wameshinda sita na kupoteza mbili ambayo pia si rekodi nzuri na imewaporomosha kwa asilimia 26 ya ubora wao.
Kwa takwimu hizo, inaonekana wazi kuwa Atetico Madrid hawabahatishi tena na wanaweza kufanya makubwa na kushinda La Liga, hasa kama watakuwa makini katika mechi zao tano za mwisho.
Ligi ya Mabingwa:
Utaona, kawaida timu za Hispania ambazo huingia hatua ya nusu fainali ni Real Madrid na Barcelona, lakini safari hii Atletico Madrid imeingia katikati na kuwaondoa vijana hao kutoka Catalunia.
Hii ni sehemu ya kuonyesha ni timu bora ya Hispania kwa kipindi hiki hasa kama itaendelea kucheza kwa kiwango sahihi bila ya kuyumba.
Atletico Madrid itacheza na Chelsea kutoka England, lolote linawezekana kwa kuwa Kocha Diego Simeone si mgeni kwa Jose Mourinho wakati akiwa Real Madrid.
Hata kama Mourinho atakuwa amehamia timu nyingine, bado ana nafasi ya kujua kipi afanye ili kupambana naye.
Kikosi hicho cha Simeone kimebakiza mechi tatu tu kuweka rekodi mpya ya kuwa Mabingwa Ulaya na kwa ubora wao ni kitu kinachowezekana kabisa.
Iwapo watafanikiwa kuchanga karata zao vizuri dhidi ya Chelsea, basi mechi ya mwisho itakuwa ni fainali dhidi ya jirani zao Real Madrid au mabingwa watetezi Bayern Munich.
Atletico Madrid si yenye majina makubwa, mkali wao Diego Costa, pia Koke lakini bado kuna wachapakazi kibao ambao hawana mbwembwe wala umaarufu na ndiyo silaha ya vijana hao wa Simeone.

LA LIGA
IMESHINDA   IMEPOTEZA  SARE  POINTI
    26                         3               4          82




  

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic