April 16, 2014

MESSI
Wachezaji tegemeo wa kikosi cha kwanza cha Simba, beki Donald Musoti na kiungo mshambuliaji Ramadhani Singano ‘Messi’, wameanza mazoezi ya pamoja na timu hiyo baada ya kuwa nje kwa muda mrefu kutokana na kusumbuliwa na majeraha.

Wachezaji hao hawakuonekana kwenye mchezo wao wa Jumapili iliyopita dhidi ya Ashanti, hali iliyowatia hofu mashabiki wa Simba kama watacheza kwenye mchezo ujao dhidi ya Yanga.

SALEHJEMBE iliwashuhudia wachezaji hao wakifanya mazoezi ya pamoja kwenye Uwanja wa Kinesi jijini Dar juzi na lilipomuuliza kocha mkuu Zdravko Logarusic kuhusiana na hali za wachezaji hao, alisema walikuwa wakisumbuliwa na maumivu ya misuli lakini kwa sasa wapo sawa na watakuwepo kwenye mchezo wa Jumamosi.

Alisema ana furaha kuona wachezaji hao muhimu wanarudi kikosini japo wamebakiwa na mchezo mmoja lakini una umuhimu mkubwa kwani wanataka kuonyesha kuwa japo wapo nafasi ya nne lakini wana uwezo mkubwa zaidi ya Yanga.
“Messi na Musoti walikuwa na maumivu ya misuli lakini daktari amethibitisha kuwa kwa sasa wapo fiti na nina uhakika watakuwepo katika mechi yetu na Yanga na mashabiki wasiwe na wasiwasi,” alisema Logarusic       

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic