April 1, 2014





Juhudi za Simba kufanya mabadiliko katika baadhi ya vipengele vya katiba yake hasa kile cha kumpa nafasi mgombea yoyote hata aliyewahi kufungwa jela kugombea, zimekwama.

Kamati ya sheria ya TFF imekikataa kipendekezo hicho ambacho kilikuwa kinaeleza mtu aliyewahi kufungwa na akarudi uraiani kwa miaka mitano bila kufanya makosa anaweza kugombea.
Awali Simba ilikuwa inaficha kuhusiana na kukataliwa kwao, lakini leo imethibitisha kuhusiana na hilo kupitia msemaji wake, Asha Muhaji.
Ilielezwa kwamba mmoja wa viongozi walio katika kamati za Simba alitaka kugombea uenyekiti, kutokana na uamuzi huo maana umezima ndoto zake.
Muhaji amesema yalikuwa mapendekezo ya wanachama na walilenga kutaka Wanasimba ambao waliingia gerezani watakuwa wamepata mafunzo kutokana na vifungo, basi wapewe nafasi.
Vipengele vingine vimekubaliwa na kamati hiyo ya sheria ya TFF na vimepelekwa kwa msajiri kwa ajili ya kupitishwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic