April 1, 2014




Gumzo la uzembe wa kipa Juma Kaseja na beki Kelvin Yondani kusababisha Yanga kufungwa na Mgambo Shooting kwa mabao 2-1, limezimwa na uongozi wa klabu hiyo.

Mashabiki  na wanachama wa Yanga walionyesha kuchukizwa na Kaseja na Yondani na kusema ndiyo waliosababisha Yanga kupoteza mchezo kwa Mgambo.
Lakini Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu amezungumza leo na kusema uongozi hautaki kumlaumu mtu na badala yake unaendelea kupamabana.
“Inawezekana hata Azam FC nayo ikateleza, hivyo tunaendelea kupambana hadi mwisho wa ligi ndiyo tutajua kama tumeshindwa au la.
“Hatupaswi kulaumiana sasa maana ni mapema sana, hivyo tunasisitiza vita bado ni mbichi na sisi tumekuwa tukijipanga kuendelea kutafuta ushindi.
“Hatujui wenzetu wanatumia njia gani lakini na sisi tuna njia zetu ambazo tunatumia kwa ajili ya kupata ushindi,” alisema Njovu.
Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga, Yanga ilifungwa bao la kwanza babada ya Kaseja kushindwa kuondoa mpira aliorudishiwa na Yondani na bao la pili, Yondani akamuangusha mchezaji wa Mgambo ndani ya eneo la hatari na kusababisha penalty.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic