April 2, 2014


Mashabiki wa matawi mbalimbali ya Simba wamekutana na kufanya kikao ambacho kwa pamoja wamekubaliana kutokwenda uwanjani na mabango wala morali kubwa ya ushangiliaji isipokuwa kwenye mechi ya mwisho dhidi ya Yanga pekee.
Kikao hicho na mjadala huo vimetokana na matokeo mabaya mfululizo ya timu hiyo kwenye mechi zake za ligi ambapo kabla ya kikao hicho tayari uhudhuriaji wa mashabiki hao kwenye mechi za Simba zinazopigwa katika Uwanja wa Taifa, Dar , ulishuka maradufu ikilinganishwa na idadi ya misimu iliyopita.


Masoud Hassan ‘Ustaadh’,  ambaye ni Mwenyekiti wa Tawi la Mpira Pesa lililopo Magomeni, amesema  kikao hicho kilifanyika wiki iliyopita kabla ya mechi ya Simba na Azam iliyopigwa Jumapili.

Katika mechi hiyo uwanjani kulikuwa na bango moja tu la mashabiki na hakukuwa na kikundi chochote cha ushangiliaji,  jambo ambalo lilizua wasiwasi mkubwa.
“Kutokana na mwenendo mbovu wa timu, tumekubaliana kutokwenda uwanjani na mabango yale yanayoonyesha hili ni tawi fulani kama ilivyozoeleka, isipokuwa tutafanya hivyo kwenye mechi tutakayocheza na Yanga pekee kwa kuwa hiyo ni mechi muhimu sana kwetu.
“Mashabiki wanakwenda uwanjani lakini si kwa idadi ile ya awali kwa kuwa wengi wao wamesusa kutokana na haya matokeo. Sasa hivi tumeelekeza nguvu zetu kumuangalia kiongozi atakayetufaa kwa ajili ya mafanikio kwenye uchaguzi unaokuja.
“Tutaanza tena kuja na mabango msimu ujao kwa kuwa tutakayemchagua tutakuwa na imani naye ya kuturejesha uwanjani kuishangilia timu yetu kama ilivyokuwa awali,” alisema Masoud.

Matawi yaliyohudhuria kwenye kikao hicho ni pamoja na Tawi la Mpira Pesa, Ubungo Terminal, Vuvuzela, Wekundu wa Msisiri, Wekundu wa Keko na Wekundu wa Mchikichini

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic