June 19, 2014

MKURUGENZI MTENDAJI WA BIN SLUM TYRES, BIN SLUM AKIONYESHA JEZI ZITAKAZOTUMIWA NA NDANDA FC KATIKA LIGI KUU BARA ZIKIWA NA CHATA YA VEE RUBBER.
Kampuni ya Binslum Tyres Limited imeweka rekodi mpya katika soka nchini baada ya kuingia mkataba na timu ya tatu inashiriki Ligi Kuu Bara.

Leo kampuni hiyo imeingia mkataba wa mwaka mmoja na Ndanda FC ya Mtwara kwa ajili ya kuidhamini katika kuelekea msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

Maana yake Binslum Tyres sasa itazidhamini timu tatu za Ligi Kuu Bara ambayo ni rekodi kwa kampuni binafsi kudhamini timu tatu tofauti, kutoka mikoa mitatu tofauti na yote mitatu kutoka nje ya Dar es Salaam.
Kampuni nyingi zimekuwa zikivutiwa kuzidhamini timu za soka kutoka mkoani Dar es Salaam, lakini Binslum Tyres imeleta mapinduzi.
Huo ni udhamini wa tatu kwa kampuni hiyo kwa timu shiriki za ligi kuu, nyingine ni Mbeya City na Stendi United iliyopanda daraja kwa ajili ya msimu ujao.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Nassor Bin Slum alisema kuwa udhamini huo umegharamia kiasi cha shilingi milioni 50 kwa kipindi hicho.

Binslum alisema, lengo la kudhamini timu hizo ni kujiweka pamoja na wateja wao ambayo kiasi kikubwa yamefanikiwa kwa kiwango kikubwa kutokana na kuanza udhamini wao Nyanda za Kusini, Nyanda za Kaskazini, Nyanda za Kati, Zanzibar na Pemba.   
 Awali Binslum Tyres ilikuwa ikijotolea kuisaidia Coastal Union ambayo mkurugenzi wake ni shabiki mkubwa wa klabu hiyo.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic