June 27, 2014



UCHAGUZI Mkuu wa Klabu ya Simba unatarajiwa kufanyika keshokutwa Jumapili, mmoja wa wagombea katika uchaguzi huo ni Ally Suru.


Suru anayewania nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba amezungumza na gazeti hili na kueleza kuhusu mipango yake, ambapo kauli mbiu yake ni ‘Ushindi Kwanza’.

Suru ambaye ana Shahada ya Uzamili ya Fedha na Uwekezaji (MSc-Finance & Investment) aliyoipata katika Chuo Kikuu cha Coventry, Uingereza, amewaahidi Wanasimba yafuatayo:

“Kubwa nitakaloanza nalo baada ya kuingia madarakani, ni kuboresha timu, maana kwa muda wa miaka miwili iliyopita timu yetu imepoteza hadhi.

“Kuimarisha timu ya vijana pia itakuwa moja za kazi zangu kubwa, ili kupata timu bora ya wakubwa ni lazima uwekeze kwa vijana wenye vipaji.

“Jambo jingine ni ujenzi wa kituo cha michezo ili kuhakikisha klabu yetu inakuwa na uwanja wake, awamu ya kwanza ni ujenzi wa uwanja wa mazoezi na hosteli, ambao ni mpango wa muda mfupi.

“Awamu ya pili ni mkakati wa ujenzi wa uwanja wa kudumu ili kuiwezesha klabu yetu iweze kumiliki uwanja wake binafsi wa kiwango cha kisasa.

“Lakini pia kuna umuhimu wa klabu kuwa na akaunti mbili; ya kawaida na ya maendeleo kwani taasisi zote duniani ambazo zimefanikiwa zimekuwa na huu utaratibu kwa kutofautisha fedha za matumizi na zile za maendeleo.

“Kuongeza wanachama pia ni moja ya silaha za maendeleo, rasilimali watu ni muhimu sana, mfano tukiwa na wanachama 100,000 wanaolipa ada kwa mwaka tutaweza kukusanya jumla ya shilingi bilioni 1.2 kwa mwaka.”

Suru pia pia ana shahada nyingine ya uhasibu kutoka Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), amewahi kuwa kiongozi wa nyadhifa zifuatazo; Mwenyekiti wa Michezo Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi hadi sasa, Mjumbe wa Mkutano Mkuu Shimiwi Taifa hadi sasa, Makamu Mwenyekiti wa Michezo Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic