Kocha
mpya wa Yanga, Marcio Maximo amewataka wadau kuvuta subira katika mambo
atakayoanza kufanya kwa kuwa soka yanahitaji subira.
“Ndiyo
maana sikutaka kuzungumza hadi kutakapokuwa na mkutano wa waandishi, baadaye
nitaanza kazi.
“Hivyo
waambie watu wote, Wanayanga, waandishi na wengine wawe na subira kwa kuwa niko
Yanga sasa kwa miaka miwili,” alisema Maximo.
Maximo
ametua Yanga ambayo ameingia nayo mkataba wa kuinoa kwa miaka miwili sambamba
na msaidizi wake Leonardo Leiva Martins.
Maximo anatarajia kuwa na mkutano na waandishi wa habari leo kwenye makao makuu ya Yanga jijini Dar es Salaam.
0 COMMENTS:
Post a Comment