June 15, 2014


 Siku chache zilizopita niliandika makala kuzungumzia namna kampuni kama ile ya Bin Slum Tyres inavyoweza kupewa sapoti.




Kabla ya kuanza msimu ujao, tayari kampuni hiyo imesaini mkataba wa kuzidhamini timu za Ligi Kuu Bara.
Ilianza na Mbeya City, mkataba wa miaka mitatu wenye thamani ya Sh milioni 360, si mchezo.

Ikaibuka tena ikasaini mkataba wa Sh milioni 50 kwa mwaka na Stand United ya Shinyanga.

Nimesikia huenda ikasaini na timu nyingine tena ya Ligi Kuu Bara. Ningekuwa Mwingereza ningesema: “What a support.”
Hata kama inatafuta kujitangaza, lakini Bin Slum Tyres imeonyesha mapenzi makubwa kwenye mchezo wa soka, kudhamini hadi timu iliyopanda daraja.

Timu kuwa na nguvu kifedha ni kuongeza ushindani wa mchezo huo na kuusaidia kukua.
Hivyo nikasema wanaopenda soka, wanaweza kwenda kununua bidhaa za Bin Slum ili kampuni hiyo ione haikukosea kuingia kwenye soka ili iendelee kudhamini, maana yangu hivi isije ikakimbia maana inahitajika.
Leo asubuhi, Mwenyezi Mungu kanijaalia afya njema, nimekwenda kwa Bin Slum kununua matairi pamoja na betri.
Matairi nitaweka kwenye gari moja, betri kwenye gari jingine, lengo hapa si kutaka kukutaarifu nina gari zaidi ya moja, badala yake kukuonyesha nilichoandika si maneno tu, badala yake hata vitendo.
Nimeanza, ninaamini wengine wanaopenda mchezo wa soka, iwe kutokea mkoani Mbeya, Shinyanga au Dar es Salaam na mikoa mingine waungeni mkono wafanyabiashara wanaokubali kuingiza fedha zao kwenye soka na kusaidia.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic