June 16, 2014




Kila mpenda mpira hasa watu wa mazoezi angependa kuwa na mwili uliogawanyika kama ule wa Cristiano Ronaldo.
Unakumbuka alipofunga bao la nne dhidi ya Bayern Munich kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, akatunisha misuli, si mchezo.


Lakini si lahisi kuwa kama yeye, maana taarifa zimevuja kuwa pamoja na mazoezi mengine huwa analiinua gari aina ya Toyota Prius mara 16.
Lengo la kufanya hivyo ni kujenga mwili wake zaidi na kweli anaonekana kufanikiwa.
Pia imeelezwa kuwa Ronaldo amekuwa akifanya yale mazoezi ya tumbo, kulala na kuamka mara 3,000!
Pamoja na hivyo anakuwa kwenye mpangilio mzuri wa chakula au diet na anakula zaidi vyakula vyenye protini na cabohydrates, pia amekuwa akilala kwa saa nane kila siku.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic