July 2, 2014


Na Eddie Salim
Ijumaa 04/07/2014, Wenyeji Brazil wataikaribisha Colombia katika Robo fainal ya kwanza. Wabrazil na wanaoipenda Brazil wataelekeza mikono yao juu kusali na kuomba dua timu yao ishinde.
Kama walivoelekeza siku waliyocheza na Chile ilipokosa bao la wazi katika dakika za mwisho kabla ya matuta.


Brazil mpaka sasa haikuonyesha kiwango chao cha kweli,ila kadiri wanavosonga mbele timu itakua inapafom uzuri. ila mechi ya Colombia haitakua lelemama kwani mpinzani ameshinda mechi zake zote nne na ina mfungaji mzuri mno ambaye mpaka sasa amefunga mabao 5.

Pia mpinzani inacheza as team, pia siku ya ijumaa watakua hawana presha kama inavyo Brazil. Kwa mtu yoyote anayefuatilia Brazil anajua wazi kua Brazil wanamtegemea sana Neymar, ambaye Ijumaa wa Colombia hawatamuachia acheze anavotaka.

Hapa itabidi wenzake wamtue mzigo kwa hio akina Hulk na Fred watabidi wae tayari kwa kufanya kazi ya ziada.

Brazil ya mwaka huu haina jina zito ambalo linawashtua wapinzani wao kama hapo nyuma,hii inatokano na ukaidi wa Scolari kama alivofanya mwaka 2002 alivokataa mwito wa Raisi wa Brazil alipotakiwa amchukue Romario,ila wakati ule Brazil ilikua inavifaa kama Gaucho,Rivaldo na Ronaldo.

Ninavyona angemchukua mmoja kati ya watatu hawa timu ingekua na uzito na ukali ziada. Kama angekua supa sub zaidi ya Benard- with my respect- Gaucho angekua bomba  mbele kuliko Jo-with my respect to Jo- au hata Bato nae angesaidia.
angemuingiza mmoja kati ya hawa pale timu inapo hitaji uzoefu na uwezo.

Mwisho kabisa nnawatakia mechi nzuri katika robo fainal zote kwani waliofika stage hii ndio wanaoujua mpira,na waliotolewa wangojee mpaka 2018 kwenye uhai.  KILA LA HERI SELECAO....ABRIGADO BRAZIL!!!!!!!!!

MWANDISHI WA MAKALA HAYA NI MSOMAJI WA BLOG HII.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic